Home Podcasts MAELEZO PODCASTS
MAELEZO PODCASTS

MAELEZO PODCASTS

Tanzania Information Services Department (Idara ya Habari-MAELEZO) 11 Episodes Jul 17, 2026

Sikiliza MAELEZO PODCASTS (Podcasts za Kiswahili kutoka Idara ya Habari MAELEZO, Tanzania) kupata taarifa na matukio mbalimbali nchini Tanzania. Idara ya Habari (MAELEZO) ipo chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ikiwa na jukumu la kutoa taarifa kuhusu utekelezaji wa Sera, mipango na miradi ya maendeleo vinavyotekelezwa na Serikali kwa wananchi, kusimamia vyombo vya habari hasa magazeti na machapisho na kuishauri Serikali juu ya Sera na Sheria za habari.

Episodes

Tiba ya Upandikizaji wa Uume kwa Wanaume
Tiba ya Upandikizaji wa Uume kwa Wanaume Jul 17, 2026 3017 Dkt. Rugakingira kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma anatupitisha kwenye huduma hii iliyojizolea umaarufu ya upandikizaji wa uume kwa wanaume wenye changamoto za uzazi. Amejibu kuhusu nani anaweza kupandikiziwa uume, gharama na matarajio baada ya huduma.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali
Ukweli Kuhusu Faida za Vyama vya Ushirika
Ukweli Kuhusu Faida za Vyama vya Ushirika Jul 13, 2026 2752 Mazungumzo na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika kutoka Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania, Bw. Florian Haule kuhusu ushirika na ukweli wake vile umesaidia kuinua uchumi wa Watanzania tangu zamani hadi sasa.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali
Fursa kwa Watanzania Kuelekea AFCON 2027
Fursa kwa Watanzania Kuelekea AFCON 2027 Jul 10, 2026 2347 Kuelekea Michuano ya AFCON 2027 ambayo Tanzania anatarajiwa kuwa mwenyeji wa michuano hii mikubwa Barani Afrika, tumemualika Bw. Allan Allex, Afisa Michezo Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Michezo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Afisa Programu wa Baraza la Michezo la Afrika Kanda ya Nne.Tumezungumza kuhusu fursa zilizopo, zinazoendelea kujitokeza na zinazotarajiwa kujito
Siri ya Tarehe 7 Julai na Historia ya Tanzania Iliyowafanya UNESCO kuichagua kuwa Siku ya Kiswahili Duniani
Siri ya Tarehe 7 Julai na Historia ya Tanzania Iliyowafanya UNESCO kuichagua kuwa Siku ya Kiswahili Duniani Jul 6, 2026 2569 Mazungumzo na Profesa Rehema Erasto., Mhadhiri wa Kiswahili kutoka Idara ya Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma kuhusu historia ya siku ya Kiswahili Duniani, nafasi ya lugha za kijamii (makabila), makosa kwenye lugha ya kiswahili na namna ya kusahihisha.Mazungumzo haya yanapatikana pia kupitia chaneli ya Youtube ya Maelezo TV.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali
Kwanini Kongamano la Kiswahili Ufaransa na si kwingine? Majibu ya Msemaji Mkuu wa Serikali
Kwanini Kongamano la Kiswahili Ufaransa na si kwingine? Majibu ya Msemaji Mkuu wa Serikali Jun 30, 2026 1775 Gerson Msigwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo; na Msemaji Mkuu wa Serikali akitoa majibu ya ni kwanini Kongamano la Kiswahili la Pili la Kimataifa limefanyika nchini Ufaransa na si kwingineko.Pia tumezungumzia asili ya makongamano ya kiswahili ya kimataifa, fursa na ushiriki wa wananchi katika makongamano haya.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali
Kuelekea Kongamano la Pili la Kiswahili la Kimataifa, Paris - Ufaransa
Kuelekea Kongamano la Pili la Kiswahili la Kimataifa, Paris - Ufaransa Jun 18, 2026 2052 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inatarajia kufanya Kongamano la pili la kimataifa la Kiswahili kati ya Julai 4 - 7, 2026, jijini Paris, Ufaransa.Tumezungumza na Bw. Tito Lulandala, Afisa Utamaduni Mwandamizi, kutoka Idara ya Maendeleo ya Utamaduni, na Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Maandalizi ya Kong
Fursa, Ushirikiano kati ya Algeria na Tanzania: Balozi Matinyi
Fursa, Ushirikiano kati ya Algeria na Tanzania: Balozi Matinyi Jun 12, 2026 439 Mheshimiwa Balozi Mobhare Matinyi akizungumza mara baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho wa kibalozi kwa Mheshimiwa Abdelmadjid Tebboune, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, katika hafla iliyofanyika kwenye Ikulu ya Algiers tarehe 10 Juni, 2026. Balozi Mobhare Matinyi anayeiwakilisha Tanzania nchini Algeria, ametoa wito kwa Watanzania kutumia fursa za ushirikiano mzuri baina
Balozi Kombo Aeleza Umuhimu wa Ziara ya Rais Samia katika Kuimarisha Mahusiano ya Tanzania na Urusi
Balozi Kombo Aeleza Umuhimu wa Ziara ya Rais Samia katika Kuimarisha Mahusiano ya Tanzania na Urusi Jun 8, 2026 1529 Mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya Kitaifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, tarehe 7 Juni, 2026.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali
Miaka 10 ya BMH: Jinsi Hospitali ya Benjamin Mkapa Ilivyobadilisha Huduma za Kibingwa Tanzania
Miaka 10 ya BMH: Jinsi Hospitali ya Benjamin Mkapa Ilivyobadilisha Huduma za Kibingwa Tanzania Jun 4, 2026 2682 Hospitali ya Benjamin Mkapa ni hospitali ya rufaa ya kanda iliyopo jijini Dodoma, iliyoanzishwa kwa lengo la kutoa huduma za kibingwa ambazo kwa sasa zipo 20 na ubingwa bobezi zipo 17 kwa wananchi wa Tanzania na nchi jirani. Tangu kuanza kutoa huduma zake, hospitali hiyo imeendelea kukua kwa kasi na kuwa miongoni mwa vituo vinavyoongoza nchini katika huduma za matibabu ya moyo, figo, saratani, upa
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 (Mei 4, 2026)
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 (Mei 4, 2026) May 27, 2026 3515 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, akiwasilisha makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Mei 4, 2026, bungeni, jijini Dodoma.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali
Hotuba ya Mhe. Rais Samia na Mhe. Rais, Paul Kagame, Mei 03, 2026
Hotuba ya Mhe. Rais Samia na Mhe. Rais, Paul Kagame, Mei 03, 2026 May 24, 2026 796 Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame, amefanya ziara ya siku moja nchini Tanzania, akizungumza na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhusu ushirikiano na kukuza uchumi wa pande zote, Mei 3, 2026.Viongozi hawa walikubaliana kuendelea kukuza biashara na uwekezaji kwa kuondoa vikwazo vya kikodi, ili kunufaika na masoko ya kikanda ya Jumuiya ya Afrika M
Hotuba ya Rais, Dkt. Samia Kwenye Kongamano la Biashara Baina ya Tanzania na Kenya, Mei 4, 2026
Hotuba ya Rais, Dkt. Samia Kwenye Kongamano la Biashara Baina ya Tanzania na Kenya, Mei 4, 2026 May 22, 2026 1331 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Kongamano la Biashara baina ya Tanzania na Kenya (Tanzania & Kenya Business Forum 2026), tarehe 04 Mei, 2026, JNICC, jijini Dar es Salaam ambapo kongamano hili lilihudhuriwa pia na Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Dkt. William Samoei Ruto.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali

Recommended