Home Podcasts Neno la Leo
Neno la Leo

Neno la Leo

Neno la Leo 255 1 Episodes Aug 12, 2026

Hii ndiyo siku aliyoifanya Bwana (Zaburi 118:24). Anza siku mpya ya Yesu kwa kusiliza na kutafakari nasi “Neno la Leo” kila siku kwa lugha ya Kiswahili.

Episodes

Usitafute Baraka Pekee, Tafuta Uwepo wa Mungu!
Usitafute Baraka Pekee, Tafuta Uwepo wa Mungu! Aug 12, 2026 1147 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo kupitia 1 Samweli 3:19 tunaona Samweli akiendelea kukua na kuingia katika kusudi lake kama nabii. Lakini Biblia inatuonyesha siri iliyokuwa nyuma ya safari yake: “Bwana alikuwa pamoja na Samweli.” Mafanikio yake hayakuanzia katika kipawa, uwezo au nafasi yake bali katika uwepo wa Mungu uliokuwa pamoja naye. Hili linatufundisha kwamba tunaweza kuwa na mipango mizuri, el
Acha Kuzungumza Tu, Jifunze Kumsikiliza Mungu!
Acha Kuzungumza Tu, Jifunze Kumsikiliza Mungu! Aug 11, 2026 583 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo kupitia 1 Samweli 3:9–10 tunafika katika moja ya nyakati muhimu sana katika maisha ya Samweli: Mungu anamwita kwa jina. Samweli alikuwa tayari akimtumikia Mungu lakini bado hakujifunza kuitambua sauti yake. Baada ya kuelekezwa na Eli, anajibu, “Sema, kwa maana mtumishi wako anasikiliza.” Kupitia simulizi hii tunajifunza kwamba uhusiano wetu na Mungu hauwezi kuwa sisi k
Kumuheshimu Mungu ni Njia ya Kwenda Mbele!
Kumuheshimu Mungu ni Njia ya Kwenda Mbele! Aug 10, 2026 1228 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo kupitia 1 Samweli 2:30 tunaingia katika simulizi ya familia ya Eli na kukutana na kanuni nzito kutoka kwa Mungu: “Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu.” Wana wa Eli walikuwa na nafasi ya kuheshimiwa kama makuhani lakini walitumia nafasi hiyo vibaya na kuidharau kazi ya Mungu. Kupitia maisha yao tunajifunza kwamba mbele za Mungu cheo, nafasi au kuonekana wa kiroho hakutosh
Mungu Anakuandaa Kupitia Ukuaji wa Taratibu.
Mungu Anakuandaa Kupitia Ukuaji wa Taratibu. Aug 9, 2026 611 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo simulizi linahamia kwa Samweli kupitia 1 Samweli 2:26. Kabla hajawa nabii mkubwa tunayemjua baadaye, Biblia inatuonyesha Samweli akiwa katika mchakato wa kukua, kujifunza na kupata kibali mbele za Mungu na wanadamu. Kupitia maisha yake tunajifunza kwamba Mungu hafanyi kila kitu kwa siku moja. Mara nyingi hutumia hatua ndogo za kila siku kujenga tabia, imani na uwezo tu
Mungu Bado Anaandika Sura za Hadithi ya Maisha Yako
Mungu Bado Anaandika Sura za Hadithi ya Maisha Yako Aug 8, 2026 522 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo tunaendelea na wimbo wa Hana kupitia 1 Samweli 2:6–8. Hana anaposema kwamba Bwana hushusha na kuinua, hufukarisha na kutajirisha, hazungumzi kuhusu Mungu ambaye amesikia habari zake tu. Anazungumza kuhusu Mungu ambaye amemwona akibadilisha maisha yake mwenyewe. Mwanamke aliyekuwa akilia kila mwaka huko Shilo sasa amekuwa ushuhuda kwamba hali ya leo si lazima iwe mwisho
Mungu Hupima Moyo Wako na Sio Mafanikio Yako!
Mungu Hupima Moyo Wako na Sio Mafanikio Yako! Aug 7, 2026 582 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo tunaendelea na wimbo wa Hana kupitia 1 Samweli 2:3. Baada ya Mungu kubadilisha maisha yake, Hana angeweza kutumia ushindi wake kuwajibu wale waliokuwa wamemdharau. Badala yake, anatukumbusha kwamba tusiseme kwa majivuno kwa sababu Mungu anajua yote na ndiye anayepima matendo ya mwanadamu. Kupitia maisha yake tunajifunza kutowadharau wengine kwa sababu ya hali wanayopit
Usiishie Kupokea Baraka, Mjue Mtoa Baraka!
Usiishie Kupokea Baraka, Mjue Mtoa Baraka! Aug 6, 2026 608 Leo kwenye Neno la LeoLeo tunaanza wimbo wa Hana kupitia 1 Samweli 2:1–2. Baada ya kusubiri kwa uvumilivu, kupokea muujiza na kumrudishia Mungu Samweli, Hana anafanya jambo kubwa zaidi: anamwabudu Mungu. Cha kushangaza ni kwamba wimbo wake hauzungumzi sana kuhusu mtoto aliyempata bali kuhusu ukuu, utakatifu na uaminifu wa Mungu. Kupitia simulizi hii tunajifunza kwamba lengo la mwisho la baraka si
Subiri kwa Amani, Kisha Mpe Mungu Utukufu!
Subiri kwa Amani, Kisha Mpe Mungu Utukufu! Aug 5, 2026 1100 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo tunahitimisha simulizi ya Hana kupitia 1 Samweli 1:27–28. Baada ya kusubiri kwa imani na kupokea amani kabla ya jibu, Hana anashuhudia uaminifu wa Mungu na anarudi mbele zake kutimiza ahadi yake. Hakuliona jibu la maombi yake kama mafanikio yake binafsi bali kama zawadi kutoka kwa Mungu, hivyo akamrudishia Mungu kile alichokuwa amempa. Kupitia simulizi hii tunajifunza
Wakati wa Mungu!
Wakati wa Mungu! Aug 4, 2026 1046 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo tunaendelea na simulizi ya Hana kupitia 1 Samweli 1:20. Baada ya kipindi kirefu cha kusubiri, machozi na maombi, wakati wa Mungu ulifika. Hana akapata mtoto wa kiume aliyemwita Samweli, akisema, “Kwa sababu nilimwomba kwa Bwana.” Kupitia simulizi hii tunajifunza kwamba Mungu hachelewi wala hasahau ahadi zake. Anapokuwa kimya, mara nyingi huwa anaandaa jambo kubwa zaidi
Mungu Hukupa Amani Kwanza Kabla ya Majibu!
Mungu Hukupa Amani Kwanza Kabla ya Majibu! Aug 3, 2026 855 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo tunaendelea na simulizi ya Hana kupitia 1 Samweli 1:17. Baada ya kumimina moyo wake mbele za Mungu, Hana anapokea maneno ya kuhani Eli: “Nenda kwa amani.” Cha kushangaza ni kwamba hali yake ilikuwa bado haijabadilika, lakini moyo wake ulikuwa umebadilika. Kupitia simulizi hii tunajifunza kwamba Mungu mara nyingi hutupa amani kabla ya kutupa jibu la maombi yetu. Tunapom
Maombi Yanaweza Kubadili Historia.
Maombi Yanaweza Kubadili Historia. Aug 2, 2026 826 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo tunaendelea na simulizi ya Hana kupitia 1 Samweli 1:10–11. Akiwa na uchungu mkubwa moyoni, Hana hakukata tamaa wala hakulipiza kisasi kwa waliomdhihaki. Badala yake, alimimina moyo wake mbele za Mungu kwa maombi ya dhati na akaweka nadhiri ya kumrudishia Mungu kile ambacho angekipokea. Kupitia simulizi hii tunajifunza kwamba Mungu husikia maombi yanayotoka katika moyo
Ni Mungu Pekee!
Ni Mungu Pekee! Aug 1, 2026 623 🎙️ Leo kwenye Neno la LeoLeo tunaanza simulizi ya Hana kupitia 1 Samweli 1:1–8. Hana alikuwa akipendwa sana na Elkana, lakini bado moyo wake ulikuwa umebeba maumivu ambayo hakuna mwanadamu angeweza kuyaponya. Kupitia simulizi hii tunajifunza kwamba kuna mahitaji ya ndani ambayo hayawezi kutimizwa na upendo wa watu, mafanikio au mali, bali na Mungu pekee. Je, tunampelekea Mungu kilio cha mioyo yetu

Recommended