
TANAPA PODCAST
Huu ni podikasti rasmi ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA). Tunachunguza mazungumzo muhimu kuhusu elimu ya uhifadhi, utalii, na fursa za uwekezaji katika Hifadhi za Taifa za Tanzania. Kila kipindi kinaangazia mikakati ya uhifadhi endelevu na ushirikiano muhimu unaosaidia kulinda maliasili zetu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Episodes

S02 EP02 - Ujirani Mwema na Faida Zake kwa Jamii
Katika episodi hii utasikia simulizi, uzoefu na ushuhuda kutoka kwa wataalamu wa uhifadhi pamoja na wanufaika wa programu za ujirani mwema, wakieleza namna uhifadhi unavyochangia maendeleo ya wananchi na ustawi wa jamii.Eneo: ArushaMwongoza Kipindi:Afisa Uhifadhi Daraja la Pili, Happiness SamWageni: Afisa Uhifadhi Mwandamizi Lameck Matungwa – Kitengo cha Ujirani Mwema, Hifadhi ya Taifa Milima Mah

Promo S02 EP02 - Zifahamu faida za ujirani mwema zitokanazo na uhifadhi kwa jamii
Jamii zinazozunguka Hifadhi za Taifa zinanufaikaje na uhifadhi? Sikiliza simulizi na uzoefu wa wadau wa uhifadhi kuhusu namna ujirani mwema unavyochangia maendeleo ya wananchi na uhifadhi endelevu.TANAPA Podcast – Msimu wa 2 | Episodi ya 02Mwongoza kipindi: Happiness Sam (Afisa Uhifadhi Daraja la Pili)Wageni:• Lameck Matungwa – Afisa Uhifadhi Mwandamizi, Kitengo cha Ujirani Mwema, Hifadhi ya Taifa

SO2 EP 01: FAHAMU ELIMU YA UJIRANI MWEMA NA FAIDA ZAKE KATIKA UHIFADHI NA JAMII
Episodi hii inaangazia - Chimbuko la Elimu ya Ujirani Mwema- Uanzishwaji na malengo yake kwa jamii zinazoishi kuzunguka Hifadhi za Taifa- Faida zake na umuhimu wa ushiriki wa wananchi katika kuhifadhi rasilimali za Taifa kwa kizazi cha sasa na kijachoMgeni Mualikwa: Afisa Uhifadhi Mwandamizi Samwel Nassari, Kitengo cha Uhifadhi – TANAPA Makao Makuu.Host: Afisa Uhifadhi Daraja la Pili Happiness Sam

Promo S02 EP01 Ujio wa Msimu wa II wa Podcast
TANAPA PODCAST | SEASON IITumerejea na msimu mpya wenye simulizi, maarifa na mazungumzo yanayokupeleka karibu zaidi na ulimwengu wa uhifadhi, utalii na uwekezaji katika Hifadhi za Taifa 21 za Tanzania.Tegemea vipindi vilivyoboreshwa, maudhui ya kina, wageni mbalimbali na uzoefu mpya wa kusikiliza.TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.

S01 EP16 - MILA, DESTURI NA TAMADUNI KATIKA UHIFADHI WA MALIASILI.
Episodi hii inaangazia njia za asili zilizotumika katika utunzaji wa maliasili kwa kufuata taratibu za kitamaduni, mila, desturi na makatazo mbalimbali yaliyosaidia kusimika mizizi imara na kuwa chimbuko la uhifadhi wa kisasa. Hekima za mababu zetu kama vile kuheshimu misitu, kutotumia rasilimali kupita kiasi, na kutambua uhusiano wa binadamu na mazingira vimekuwa dira muhimu inayoongoza mbinu za

S01 EP15 - UHIFADHI NI JUKUMU LA KILA MMOJA
Episodi hii inakuletea uchambuzi wa kina kuhusu Uhifadhi kwa kuzingatia kuwa Uhifadhi wa wanyamapori ni zoezi la kujitolea kulinda na kuhifadhi maliasili kwa maslahi ya Taifa kwa kizazi hiki ma kijacho.Sikiliza Episodi ya 15 upate elimu kutoka kwa Mzee Ibrahimu Kasontola kutoka katika kijiji cha Lukoma wilayani Uvinza - Kigoma aliyejitolea kwa hali na mali kuhifadhi msitu katika eneo la makazi yak

S01 EP14 - MILA, DESTURI NA TAMADUNI KATIKA UHIFADHI WA MALIASILI.
Episodi hii inaangazia mila, desturi na tamaduni katika uhifadhi wa maliasili, hususan namna jamii ya Wangoni kutoka mkoani Ruvuma ilivyotumia majina na utamaduni wao kulinda Wanyamapori na Misitu tangu enzi za mababu zetu.Hadithi hii ya kuvutia inaonesha jinsi urithi wa jadi ulivyokuwa chachu ya kulinda rasilimali za Taifa ambazo leo hii zinachangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ya uhifadhi na

S01 EP13 - Mila na Tamaduni zilizohusisha mizimu katika kuhifadhi Maliasili
Episodi hii inakuletea mazungumzo ya kina kuhusu mila, tamaduni na makatazo ya Kabila la Wagongwe lililopo mkoani Katavi na jinsi taratibu hizo zilivyochangia kulinda maliasili na vyanzo vya maji. Mathalani; ilikuwa hairuhusiwi kukata miti iliyokuwa katika vyanzo vya maji kutokaana na imani ya kuwepo kwa nyoka mkubwa wala kuua mnyamapori hadi upewe kibali na pepo au jini Katabi anayepatikana katik

S01 EP12 - Zoezi la Uhamishaji Tembo kutoka Misenyi kwenda Hifadhi ya Taifa Burigi - Chato.
Episodi hii imeangazia zoezi endelevu la kuwahamisha tembo walowezi kutoka maeneo ya karibu na wananchi kwenda hifadhini na zoezi zima la kuwaswaga tembo waliotoka hifadhini kuvamia maeneo ya wananchi na kuwarudisha hifadhini.Sikiliza Episodi hii kwa taarifa hiyo na mengine mengi kupitia Epsode ya 12.Eneo: Misenyi - Bukoba.Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine MbenaGuests: Kamishna Msaidi

S01 EP11 - Nyumba ya Kumbukizi ya Mwl. Nyerere na Historia ya Taifa letu.
Kuelekea Kumbukizi ya Kifo cha Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere Oktoba 14, TANAPA PODCAST tunakueletea uchambuzi kuhusu historia ya harakati za uhuru wa Tanganyika zilizoongozwa na Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere. Hapa utapata kujifunza mengi kuhusu harakati za Uhuru wa Tanganyika na Afrika kwa ujumla.Ikumbukwe historia hii imehifadhiwa katika Nyumba ya Kumbukizi ya M

S01 EP10 - MAANDALIZI YA TWENZETU KILELENI 2025 NA PROF. KAMUZORA
Episodi hii inaangazia mazungumzo ya kina kuhusu zoezi la upandaji wa Mlima Kilimanjaro ambapo Profesa Kamuzora anaeleza uzoefu wake katika kupanda mlima kwa muda mrefu.Fahamu faida ya kushiriki kampeni ya “Twenzetu Kileleni katika kuadhimisha kumbukumbu ya uhuru wa Taifa letu, kuhamasisha utalii pamoja na utunzaji wa mazingira.Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena - Mkuu wa Kitengo

S01 EP09 - YAFAHAMU MAENEO YA MALIKALE YALIYOKASIMISHWA TANAPA
Episodi hii inaangazia maeneo ya Malikale yanayosimamiwa na TANAPA na faida zake.Maeneo hayo yamebeba historia za kale, biashara ya utumwa, utawala wa machifu, ukoloni na uhuru wa Taifa letu.Sikiiiza TANAPA PODCAST Epsode 09 upate elimu ya kina kuhusu historia ya Taifa letu, asili na umuhimu wa kutunza tamaduni zetu.Eneo: Dar es Salaam.Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena.Guest: Af

S01 EP08 - MAANDALIZI YA TWENZETU KILELENI 2025 NA CDF (Mst.) GEORGE WAITARA
Katika Episode hii tunaangaIa mazungumzo ya kuhusu Kampeni ya Twenzetu Kileleni 2015 inayofanyikaga Desemba 09 kila mwaka kukumbuka mashujaa wetu waliopigania uhuru wa Tanganyika ambapo kwa mwaka huo huo bendera ya Taifa ilipandishwa Mlima Kilimanjaro wenye kilele kirefu kuliko vyote Barani Afrika chenye urefu wa mita “5985 asl” kuangazia nuru ya Uhuru ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.Sikiliza T

S01 EP07 - Uchambuzi wa maneno yenye mkanganyiko katika Sekta ya Uhifadhi na Utalii
Episodi hii inaangazia uchambuzi wa kina kuhusu maneno mbalimbali yanayoleta mkanganyiko wa maana na matumizi yake katika jamii.Katika Episode 07 Mtopezi wa lugha ya Kiswahili kutoka Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) Ndugu Oni Sigala anachambua na kudadavua maneno kadha wa kadha yenye utata katika sekta ya uhifadhi na utalii.Eneo: Dar es salaamMwongozaji: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catheri

S01 EP06 - Mila, Desturi na Tamaduni katika Uhifadhi wa Maliasili
Sikiliza Episode 06 uchambuzi wa kina katika mwendelezo wa mada inayoeleza elima ya Uhifadhi ikihusisha Mila, Desturi, Tamaduni na Miiko iliyozuia uharibifu wa Maliasili za Taifa ambapo moja ya maeneo hayo kwa sasa ni Hifadhi za TaifaHost: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine MbenaGuest: Naibu Kamishna wa Uhifadhi na Maendeleo ya Biashara, Massana Mwishawa.

S01 EP05 - Mila, Desturi na Tamaduni katika Uhifadhi wa Maliasili
TANAPA Podcast Episode 05 inaangazia mwendelezo wa mada inayoeleza elimu ya Uhifadhi iliyohusisha Mila, Tamaduni, Desturi na Miiko anuwai iliyozuia baadhi ya wanyamapori kuuwawa lengo likiwa ni kuhifadhi maliasili zilizokuwa ndani ya maeneo yaliyohifadhiwa ambayo baadhi yake kwa sasa ndio Hifadhi za Taifa tunazozishuhudia zikitiririsha nyomi ya watalii nchini.Eneo: Hifadhi ya Taifa SerengetiMwongo

S01 EP04 Mila, Desturi na Tamaduni zilizotumika katika Uhifadhi wa Maliasili
Episode hii inaangazia mazungumzo kati ya Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TANAPA, Catherine Mbena na Mzee Fanuel Mbise, Eliona Miley na Elikesia Akyoo kuhusu elimu ya Uhifadhi kupitia mila, desturi na tamaduni zilizotumika katika kusheshimu na kutunza maliasili zilizokuwa zimehifadhiwa.

S01 EP03 Chimbuko la Uhifadhi
Sikiliza TANAPA Podcast, Episode 03 uelimike kuhusuChimbuko la UhifadhiUanzishaji wa Hifadhi mpya na malengo yakeMaeneo matano ya Malikale yaliyokasimishwa TANAPA naUzalendo katika kutembelea Hifadhi za Taifa.Mgeni maalum: Nakaaya Sumari (Tanzania Safari Channel)Host: ACC Catherine Mbena, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano TANAPAFuatilia mfululizo huu wa elimu ya uhifadhi, utalii na mirindimo

S01 EP02 - Kazi mbalimbali zinazofanywa na TANAPA
Katika episode ya pili ya mfululizo huu, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TANAPA, Catherine Mbena anaelezea kwa kina kazi mbalimbali zinazofanywa na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) katika kuhakikisha maliasili zilizopo ndani ya hifadhi za Taifa zinaendelea kulindwa na kuhifadhiwa kwa faida ya kizazi hiki na vizazi vijavyo.

S01 EP01 Utangulizi kuhusu TANAPA na majukumu yake
Katika episode hii ya kwanza, tunazungumzia kwa kina kuhusu Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) – kuanzia majukumu yake makuu, muundo wa utendaji kazi, hadi maeneo ya hifadhi yanayosimamiwa chini ya sheria. Ni programu endelevu inayokufahamisha nafasi muhimu ya TANAPA katika kulinda maliasili na kukuza mapato yatokanayo na shughuli za utalii.











