
Radio Uinjilishaji FM (pia inajulikana kama Amani Radio FM) ni kituo cha redio cha Jimbo Kuu Katoliki Arusha kinachotangaza kwa masafa ya 100.5 FM mjini Arusha, Tanzania. Kituo hiki kinalenga kujenga na kustawisha jamii kiimani kwa kuishi Injili ya Kristo kwa matendo, kikitoa vipindi vya kiroho, habari na elimu kwa jamii ya Arusha na Watanzania kwa ujumla.