
Blessed Hope Radio FM Stereo ni kituo cha redio cha Kikristo kwaajili ya Uinjilisti, Umisheni na Ufuasi, kilichoanzishwa na Tanzania Assemblies of God (TAG). Kipo mkoani Geita na kinatoa vipindi vya Habari, Elimu, mafundisho ya kiroho na burudani masaa 24 kila siku, siku saba kwa wiki, kikiwafikia wasikilizaji wa Geita na maeneo jirani kama Mwanza na Biharamulo.